Mapitio ya Rasimu ya taarifa ya nchi ya utekelezaji wa mkataba wa Africa wa Haki za Binadamu na watu ( African Charter on Human and People’s Right) pamoja na itifaki ya Haki za wanawake Africa ( Maputo protocal)

Leo machi 19   THRDC imeshairiki katika kikao kazi  cha kupitia rasimu  ya taarifa ya nchi ya utekelezaji wa mkataba  wa Africa wa Haki za Binadamu na watu pamoja na itifaki ya Haki  za wanawake Africa.

Kikao hiki kinafanyika Mkoani Dar Es Salaam kwa siku tatu kuanzia tarehe machi 19-21, 2025 ambapo Mgeni rasmi katika kikaohicho alikuwa  alikuwa waziri wa katiba na sheria   Mheshimiwa Damas Ndumbaro akiambatana  na Mkurugenzi msaidizi  idara ya haki za binadamu kitengo cha utoaji taarifa  Bi. Beatrice kitengo, makamu wa Tais wa TLS Bi. Letitia Mtagazwa na Dr Deus Mkiza  mwakilishi wa jukwaa la habari  la  wahariri Tanzania.

Mheshimiwa Waziri katika kutoa hotuba yake alizungumzia   Kuwa serikali imeona umuhimu wa ushirikishwaji wa wadau mbalimbali  wakiwemo waandishi wahabari, CSOs,  watu wenye ulemavu na wadau wengine wa masuala ya haki za binadamu kote  Tanzania bara na Zanzibar katika mchakato huu muhimu wa kupitia rasimu  ya taarifa ya nchi ya utekelezajiw wa mkataba wa Africa wa haki za binadamu na watu ( ACHPR) na itifaki ya haki za wanawake Africa.

Aliekeza kuwa Tanzania inatekeleza maagizo ya mikataba  ya kimataifa  ya haki za binadamu na sheria za nchi kwa kupitia 4Rs ambayo hii imekuwa Falsafa ya  Mheshimiwa Rais  wa awamu ya Sita Dr. Samia Suluhu Hassani.
 
Mh. waziri alisema wazi kuwa yapo mambo mengi ambayo tukiyaangalia yanaonyesha utekelezwaji wa haki za binadamu  nchini  yakiwemo;
•⁠  ⁠uwepo wa ibara za haki za binadamu katika katiba ya jamuhuri ya muungano wa Tanzania ( Bills of rights)
•⁠  ⁠⁠Tume ya haki za binadamu na utawala bora
•⁠  ⁠⁠usaji na uwepo wa asasi za kiraia  nchini,
•⁠  ⁠⁠nchi ku saini  na kuridhia mikataba ya kimataifa ya haki za binadamu,
•⁠  ⁠⁠Uwepo wa  mhimili wa mahakamana uhuru wake katika kutoa maamuzi,
•⁠  ⁠⁠uwepo wa mahakama za kimataifa za haki za binadamu  nchini kwetu,
•⁠  ⁠⁠Utoaji wa taarifa za utekelezaji wa haki za binadamu nchini,
•⁠  ⁠⁠Kuundwa kwa mama samia legal aid kampeni na vingine vingi.

Alisisitiza kuwa mapitio haya yatazingatia katika kuangalia haki zote zikiwemo haki za kiuchumi, kiraia, kijamii, na za kisiasa kwa muktadha wa Tanzania na Africa na kuepuka kuangalia  na kutafsiri haki za binadamu kwa muktadha wa kimagharibi bila kusahau kuangalia wapi tulipotoka, tulipo na  tunapokwenda. Tukionyesha  wapi tumefanya vizurii na wapi panahitaji maboresho na maboresho pia.
 
Aliongeza kuwa  nchi yetu iruhusu watu kuishi sehemu yoyote  kulingana na sheria za nchi, na iko wazi kuwa sheria zetu za ardhi hazijatoa kibali cha umiliko wa ardhi ( no right of ownership of land but  only occupancy  or lease) hivyo basi pale inapoona wananchi wanaishi katika maeneo hatarishi kama maeneo ya hifandhi  ambapo ni hatarishi kwa usalama  wa haki ya kuishi  kwa matukio kama kuuawa na  wanyama wa hifadhi, au ukosefu wa huduma za kijamii katika maeneo hayo, serikali inalojukumu la kuwahamisha na kuwapeleka sehemu salama kwa maslahi yao na maslahi ya umma kiujumla.

Alimaliza kwa kusema faida ya ujumuishwaji katika kupitia taarifa hizi za utekelezaji wa haki za binadamu nchini na kuwa na ripoti jumuishi ni kwa lengo la kukuza uwazi, Uwajibikaji kwa serikali  na wadau  wote, kukuza maendeleo ya kijamii, kiuchumi, kuwasaidia wahanga  wa ukiukwaji wa haki za Binadamu na ukatili wa kijinsia.

THRDC 19 MACHI 2025