Wadau kutoka sekta mbalimbali nchini Tanzania wamekutana jinini Dodoma kwa lengo la kutoa maoni yao na mapendekezo juu ya mswada wa Fedha wa mwaka 2024 - (Financial Bill 2024)

Leo  tarehe 23/6/2024  wadau kutoka sekta mbalimbali nchini Tanzania wamekutana jinini Dodoma  kwa lengo la kutoa maoni yao na mapendekezo juu ya mswada  wa Fedha wa mwaka 2024 - (Financial Bill 2024)
THRDC  ikiwakishwa na Mratibu wa Mtandao wakiliOnesmo Olengurumwa,  Ndugu Musa  Jonasi - Mwakilishi wa katibu Nacongo na Ms.  Charlotte Kabunga - mwakilishi THRDC kanda ya kati wameipongeza  Wizara ya fedha kwa kukubali baadhi ya mapendekezo ya AZAKI ya muda mrefu kuhusu kurekebisha kifungu cha 64 cha Sheria ya Mapato ya Kodi kwa kupanua tafsiri ya Shirika la Hisani ( charitable organization) na kuongeza tasisi za afya na mazingira katika  tafsiri hiyo  kwani ni hatua nzuri .

Katika kuwasilisha  Mapendekezo ya maboresho ya mswada  huo Wakili Olengurumwa Aliiambia kamati kuwa mabadiliko hayo bado ni madogo sana ukilinganisha na mapendekezo  ya AZAKI ambayo yamekuwa yakitolewa kuitaka tafsiri hiyo iguse maeneo yote yanayofanyiwa  kazi na AZAKI kama vile Eneo la utoaji wa msaada wa kisheria, eneo la utoaji elimu ya kupingana na ukatili kwa wanawake na Watoto, haki za binadamu na utawala bora nakadhalika.
Pia anapendekeza kamati ya maboresho ya sheria ya kodi  iwe jumuishi kwa kuwa na mwakilishi/wawakilishi kutoka  AZAKI  ili kuhakikisha hoja zao zinawasilishwa  na kwa ajili ya kuongeza maboresho katika sheria ya kodi kwani inayowagusa kwa namna moja au nyingine.

Mwenyekiti wa kamati  aliyapokea mapendekezo hayo  yaliyowasilishwa pia kwa njia ya maamdishi na kuahidi kuwa yatafanyiwa kazi, aliwakumbusha  wadau kuwa uongozi wa awamu hii umeipa sana kipaumbele Secta ya AZAKI kwani imewatengea wizara maalumu ya maendeleo ya jamii  na pia kianzisha kamati maalumu ya bunge ya maendeleo ya jamii, haya yote imaonyesha umuhimu wa secta hii ya AZAKI katika   Kukuza maendeleo ya jamii na taifa kwa ujumla.
IMETOLEWA NA THRDC
23 June 2024