DEFEND DEFENDERS, THRDC WAWAKUTANISHA WATETEZI WA HAKI ZA BINADAMU KUJADILI NAFASI ZA KIRAIA

Shirika la linaloshughulika kutetea haki watetezi wa haki za binadamu Afrika (DefendDefenders), Kwa kushirikiana na Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC), wanafanya warsha ya kuhusu nafasi za kiraia na haki za binadamu.

Warsha hiyo imeanza leo Desemba 7, hadi Desemba 10, 2022, ikifanyika kwenye ukumbi wa Giraffe Hotel jijini Dar es Salaam, na kuhudhuriwa na watetezi @euintanzania wa haki za binadamu kutoka mashirika wanachama wa THRDC, CWHRD na wadau mbalimbali.

Katika warsha hiyo ya siku nne, wadau hao wanatarajiwa kutumia fursa hiyo kujadili hali ya mazingira ya utetezi wa haki za binadamu nchini pamoja kuwapatia stadi mbalimbali watetezi hao ambazo zinaweza kuwasaidia kukabiliana na changamoto ambazo wamekuwa wakikumbana nazo.

Aidha siku ya mwisho ya Warsha hizo zinazofanyika mfululizo inatarajiwa kuhitimishwa kwa maadhimisho ya Siku Kimataifa ya Haki za Binadamu pamoja na kuhitimisha kilele cha siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia huku viongozi mbalimbali wa Serikali pamoja na wadau wa haki za binadamu zaidi ya 200 wakitarajiwa kuhudhuria.
#ClaimingSpacesTz22

Imetolea na
THRDC